Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) unatarajia kuuza miti laini na migumu katika mashamba 11 ya miti ya kupanda yanayomilikiwa na Serikali kwa msimu wa uvunaji wa mwaka wa fedha 2023/2024.
Tathmini iliyofanyika 2023/24 inaonesha bado kuna upungufu wa malighafi itakayogawanywa kwa viwanda vilivyosimikwa kutoka katika baadhi ya mashamba (Jedwali 1) ikilinganishwa na mahitaji makubwa ya viwanda hivyo. .