Habari » Publications and Reports

UUZAJI WA MITI YA MISAJI NA KWA NJIA YA MNADA /THE SALE OF STANDING TEAK TREES BY AUCTION

1.    Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) unatarajia kuuza miti aina ya Misaji yenye jumla ya meta za ujazo 10,733.56 iliyopo mashamba ya miti ya Mtibwa na Longuza mkoani Morogoro na Tanga mtawalia. Jumla ya meta za ujazo 7,898.82 na 2,834.74 zitauzwa katika shamba la miti Mtibwa na Longuza mtawalia. Miti hiyo iliyopimwa katika vitalu vyenye ujazo mdogo vitauzwa kwa mnada kwa kuzingatia kanuni ya 31 (ii) ya kanuni za Sheria ya Misitu za mwaka 2004. Miti hii ya Misaji itauzwa mahali ilipo na jinsi ilivyo na mnunuzi hatakuwa na haki ya kudai fidia baada ya mauzo.

 

2.    Kampuni au mtu binafsi  anayetaka kushiriki mauzo kwa njia ya mnada anatakiwa kuwasilisha maombi (Rejea sehemu ya 14 ya Tangazo) kwenye bahasha iliyofungwa kuonesha nia ya kushiriki mauzo kwa njia ya mnada akiambatisha leseni ya biashara, usajili wa kiwanda cha kuchakata magogo (2019/2020) au mkataba, Usajili wa biashara ya mazao ya misitu (2019/2020)  na cheti cha utambulisho wa mlipa kodi (TIN). Aidha, anatakiwa aoneshe jina la shamba,  namba ya kitalu/vitalu na ujazo anaotarajia kununua kama ilivyo kwenye jedwali namba 1 na 2 hapo chini.

 

3.    Mnada utaendeshwa hadharani wakiwepo wanunuzi wote katika ofisi za  mashamba husika. Mnada katika shamba la miti Mtibwa utafanyika siku ya Jumatatu tarehe 27 Aprili, 2020 saa 4:30 asubuhi na katika shamba la miti Longuza mnada utafanyika siku ya Jumatano tarehe 29 Aprili, 2020 saa 4:30 asubuhi. Mnada utafanyika kwa kufuata Sheria ya Misitu Sura 323.

 

4.    Kila kitalu kitanadiwa peke yake kulingana na bei na ujazo uliopo. Hata hivyo, bei ya juu iliyotolewa na mnunuzi wakati wa kufungua bahasha haitazuia wanunuzi wengine kuongeza bei zaidi ya iliyotajwa awali.

 

 

5.     Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania unawaalika wanunuzi kununua miti ya  misaji kwa njia ya mnada ambapo mnunuzi anaweza kuchagua mojawapo kati ya vitalu vifuatavyo: -

 

Na.

Jina la Kitalu

Ujazo kwa Kitalu (m3)

Bei ya kuanzia kwa kila meta za ujazo (TZS/M3)

1

LG8 - 22

261.85

630,000

2

KS12 - A11

387.95

720,000

3

KS12 - A12

343.09

720,000

4

KS12 - A13

387.95

720,000

5

KS12 - A15

299.23

720,000

6

KH10 - 10

515.37

720,000

7

KS12 - A19

158.94

720,000

8

KS12 - A22

153.30

720,000

9

KS12 - A24

171.49

720,000

10

KS12 - A30

155.57

720,000

          JUMLA

                 2,834.74

 

JEDWALI Na.1:ORODHA YA VITALU, UJAZO NA BEI KWA SHAMBA LA MITI  LONGUZA 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

JEDWALI Na.2: ORODHA YA VITALU, UJAZO NA BEI KWA SHAMBA LA MITI MTIBWA 

Na.

Jina la Kitalu

Ujazo kwa kitalu (M3)

Bei ya kuanzia kwa kila meta za ujazo (TZS/M3)

1

LR 12A

307.57

            260,000 

2

LR 12A-1

205.76

            340,000 

3

LR 12A-2

229.57

            260,000 

4

LR 12A-3

207.14

            260,000 

5

LR 12A-4

217.96

            260,000 

6

LR 12A-5

144.05

            360,000 

7

LR 12A-6

218.68

            230,000 

8

LR 12A-7

242.85

            250,000 

9

LR 12A-8

210.30

            190,000 

10

LR 12A-9

235.37

            180,000 

11

LR 12A-10

201.30

            190,000 

12

LR 12A-11

303.98

            200,000 

13

LR 12A-12

103.38

            240,000 

14

LR 12A-13

204.31

            210,000 

15

LR 12A-14

115.95

            240,000 

16

LR 12A-15

193.56

            270,000 

17

FN 64-16

167.67

            280,000 

18

FN 64-17

226.59

            310,000 

19

LR 16B-18

303.39

            330,000 

20

LR 16B-20

400.31

            370,000 

21

LR 16B-23

342.44

            310,000 

22

LR 16B-24

129.10

            330,000 

23

LR 16B-25

147.03

            300,000 

24

LR 16B-26

326.09

            260,000 

25

LR 16B-27

300.19

            210,000 

26

LR 16B-28

230.37

            220,000 

27

LR 16B-29

190.49

            240,000 

28

LR 16B-30

178.43

            180,000 

29

LR 16B-31

140.20

            330,000 

30

LR 16B-32

198.38

            280,000 

31

LR 14-33

57.04

            230,000 

32

LR 14-34

69.12

            180,000 

33

LR 14-35

69.12

            200,000 

34

LR 14-36

92.38

            210,000 

35

LR 14-37

132.22

            190,000 

36

LR 14-38

137.56

            210,000 

37

LR 14-39

158.65

            210,000 

38

LR 14-40

231.64

            200,000 

39

LR 14-41

173.43

            170,000 

40

LR 14-42

155.26

            130,000 

          JUMLA

              7,898.82

 

 

6.    Hati ya ushindi kwa mnunuzi aliyetaja kiwango cha juu kwa kila kitalu wakati wa mnada itatolewa.

 

7.    Mnunuzi atakayefanikiwa kununua miti ya misaji hataruhusiwa kusafirisha magogo nje ya nchi kwa mujibu wa kanuni ya 50(1) ya kanuni za misitu za mwaka 2004. 

 

8.    Makampuni na watu binafsi wanakaribishwa kutembelea vitalu shambani wakati wa saa za kazi kuanzia saa tatu (3:00) asubuhi hadi saa tisa (9:00) alasiri isipokuwa siku za sikukuu. Meneja wa shamba au msaidizi wake atakuwepo kwa ajili ya maelekezo zaidi. 

 

9.    Wanunuzi wanapaswa kuchukua na kusoma masharti ya uvunaji kwa kila shamba. Masharti hayo yanapatikana ofisi za shamba husika.

 

10. Bei ya kianzio kwa mita moja ya ujazo imeoneshwa katika Jedwali namba 1 na 2 hapo juu ikijumuisha ‘VAT’, ‘CESS’ na ‘LMDA’.

 

  1. Mnunuzi atakayeshinda atalipa asilimia ishirini na tano (25%) ya thamani yote ya ununuzi ndani ya siku tatu (3) baada ya mnada kufanyika. Fedha hizo hazitarudishwa. Asilimia sabini na tano (75%) iliyobaki italipwa ndani ya siku kumi na nne (14) baada ya mnada. Malipo yote yafanyike kwa kupitia mfumo wa makusanyo ya Serikali (GePG) baada ya kupewa Hati ya madai (Bill) ya mfumo kupitia Bank ya NMB, CRDB, Tigo au M-Pesa. Hati ya madai inayoonesha kiasi cha kulipa itatolewa na Meneja wa shamba husika.
  2. Mnunuzi atapaswa kuwasilisha hati ya malipo kwa meneja wa shamba husika kama uthibitisho wa malipo si zaidi ya siku tatu (3) baada ya malipo kufanyika.
  3. Mteja atatakiwa kuondoa mazao ya misitu aliyonunua ndani ya miezi miwili (siku sitini) baada ya kumaliza kulipa malipo yote kwa asilimia 100.
  4. Maombi yote yawasilishwe siku ya mauzo kabla ya saa 4:00 asubuhi. Aidha,    wanunuzi watakaochelewa kuwasilisha maombi yao kwa siku na muda uliopangwa hawataruhusiwa kushiriki katika mnada.
  5. Tangazo hili pia linapatikana katika tovuti zifuatazo za Wakala na Wizara: www.tfs.go.tz na www.mnrt.go.tz

 

ANGALIZO

Mshiriki atakayeshinda na kupewa hati ya ushindi na kisha yeye mwenyewe kushindwa kulipia mgawo huo ndani ya muda aliopewa (kadiri inavyoelezwa katika kipengele 11 cha tangazo hili) kwa sababu yoyote ile, atakuwa ametenda kosa la kuhujumu mnada na kwa makusudi kuikosesha Serikali mapato hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwemo kudaiwa fidia ya hasara itakayosababishwa na kitendo hicho chini ya Sheria ya Makosa ya Uhujumu Uchumi (Sura ya 200 marejeo ya 2002).

 

limetolewa na

KAMISHNA WA UHIFADHI

S.L.P 40832,

            DAR ES SALAAM

           13.04.2020

TANGAZO LA UUZAJ I WA MAZAO YA MISITU YALIYOPO KATIKA KITUO MENEJA WA MISITU WILAYA YA TANGA NA MAZAO YA MISITU YALIYOPO KATIKA KITUO MENEJA WA MISITU WILAYA YA TANGA

Pakua Faili: