Kuhusu Wakala

Muundo wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)

Kulingana na muundo wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania upo mgawanyiko katika maeneo makuu matatu: Makao Makuu, Kanda na Mashamba ya miti. Makao makuu inaundwa na menejimenti inayojumuisha Mtendaji Mkuu, Wakurugenzi watatu, Meneja wawili wa Vitengo vya Sheria na ugavi, Mhasibu Mkuu na Mkaguzi Mkuu wa ndani. Menejimenti ya Wakala na baadhi ya watumishi wengine wako katika jengo la Mpingo gorofa ya tatu.

Wakala pia una Meneja wa Kanda saba (7) na Mashamba ya miti 18. Vile vile Wakala umeboresha utendaji wake kupitia wilaya; ambapo Meneja wa wilaya 118 wameteuliwa na kupatiwa nyenzo za kazi. Tofauti na Kanda saba za awali za Uenezi na vikosi vya Doria za misitu chini ya Idara; Muundo unaojumuisha Kanda saba za Wakala umeboresha tija katika utendaji kwa kuimarisha uhifadhi na usimamizi wa misitu, ukusanyaji wa mapato, uenezi, na ulinzi wa misitu

Kanda za Wakala na Mashamba ya miti 
Wakala una Meneja wa Kanda saba (7). Kanda hizo ni Mashariki, Kaskazini, Kati, Kusini, Nyanda za juu Kusini, Ziwa na Magharibi. Vile vile Wakala umeimarisha utendaji katika ngazi ya Wilaya kwa kuteua na kusambaza Meneja wa Wilaya 118. Aidha katika ofisi 6 za kanda, Wakala unatumia majengo yaliyokuwa ya FBD ambayo yamefanyiwa ukarabati ili yaweze kutumika. Katika kanda ya Kusini, Wakala umekodi nyumba mjini Masasi. Aidha, wapo Meneja wa mashamba ya miti 18 ambayo ni: Buhindi, Kawetire, Kiwira, Korogwe, Longuza, Mbizi, Meru, Mtibwa, Kilimanjaro Kaskazini, Kilimanjaro Magharibi, Ruvu Kaskazini, Rondo, Rubare, Rubya, Sao Hill, Shume Ukaguru na Wini-Ifi nga. Meneja wa mashamba ya miti 15 wanatumia majengo yaliyokuwa chini ya FBD. Meneja wa Mashamba mapya wanatumia majengo yaliyopangishwa kwa Wakala au ofi si za zamani za idara ya misitu zilizotolewa na Halmashauri za Wilaya husika. Kila Meneja wa Kanda na wa shamba wana vitendea kazi kama magari, pikipiki, mitambo, kompyuta za vipakatalishi na mezani pamoja na vifaa vingine muhimu vya ofi si kwa ajili ya kufanyia kazi za Wakala. 

Pamoja na vitendea kazi kuwa vichakavu, kila Meneja ana bajeti ambayo iko kwenye mpango kazi wa kibiashara ukianisha shughuli za Wakala katika ngazi hiyo mfano, ukarabati wa majengo, barabara na ununuzi wa vitendea kazi; kama vile magari, pikipiki na matumizi mengine.

Majengo na vitendea kazi yaliyokuwa ya FBD yote yamechukuliwa na Wakala (TFS) na kwa sasa ni mali ya TFS. Hali ya majengo yote yanayotumika ni nzuri kwa vile yanafanyiwa ukarabati mara kwa mara. Aidha, Wakala una mpango wa kujenga majengo ya vitega uchumi katika miji ya Mbeya, Kibaha na Dar es Salaam. Hii ni pamoja na kukaratiba majengo ambayo yalikuwa chini ya FBD ambayo kwa sasa hayatumiki ili kuweza kutumika kama vitega uchumi vya Wakala. Majengo hayo yapo miji ya Morogoro, Moshi, Tanga na Shinyanga.

Mifumo ya Utendaji ya Wakala 
Baada ya Kuanzishwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania umeweka mifumo mbalimbali ya kimenejimenti kwa malengo ya kuongeza ufanisi wa kiutendaji, kuboresha utoaji huduma kwa wananchi na kupunguza gharama za uendeshaji wa shughuli za Wakala. Kwa sehemu kubwa Mifumo hii inaratibiwa na Kurugenzi ya Huduma na Uendeshaji Shughuli katika Wakala. Mifumo hii ni pamoja na Mwongozo wa Utendaji Kazi, Hati ya Kuanzisha Wakala, Mpango Mkakati, Mpango wa Biashara wa Mwaka, Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS), Uperembaji na Tathmini, Mkataba wa Huduma kwa Mteja na Mfumo wa Kushughulikia Malalamiko. Aidha mifumo mingine inayotumiwa na Wakala kutekeleza majukumu yake ni Mfumo wa usimamizi na uhakiki wa fedha (Integrated Financial Management System (IFMS)), Human Capital Information Management System, Masjala na Uhasibu.